Ticker

6/recent/ticker-posts

NCHI YA DHAMBI SEHEMU YA 11_15



       ( 11———-15 ) MWISHO 

                 ************
Ni siku mpya ndani ya nchi ya Toro...

  Binti mfalme Cesy na kijana Lari askari mtumishi wa mama yake, malkia Suze, walikuwa ndani ya nyumba ya bibi kizee huyo porini, wakiwa wanachoma nyama ya mifugo ya bibi huyo wakila kwenye moto

 Lari akiwa amekandwa kwa madawa maalumu ya mitishamba ili kuurudisha mwili wake sawa sawa, Cesy akiwa amegoma kabisa kurejea ndani ya jumba (kasri) lao siku hiyo akitaka kushinda na kijana Lari nje ya kasri

"Wajukuu zangu natoka kidogo ila nitachelewa kurudi naenda kutafuta dawa zangu kadhaa porini nitashinda huko!" bibi kizee aliwaambia asubuhi wakati wakichoma nyama

"Tukusindikize bibi?" Cesy aliuliza
"Hapana ninyi endeleeni kupumzika ila msisahau kunichotea maji mtoni!"

"Sawa bibi, safari njema!" Lari alijibu, bibi kizee huyo alijiandaa na kuondoka akiwaacha vijana hao wawili kama walinzi wa nyumba yake

"Twende tukachote maji saa hizi kabla jua halijawa kali" Lari alishauri
"Mimi nimechoka!" Cesy alijibu
"Basi baki nitaenda!"
"Hamna twende wote!" bintimfalme alijibu wawili hao wakabeba mtungi (ndoo) na taratibu safari ya kuelekea mtoni ikaanza huku wakitaniana njiani


  Walipofika mtoni wakatazama walipomwacha askari Jeda jana baada ya kumpiga hawakumwona maana walihisi alikufa, Cesy alitangulia mtoni taratibu, Lari akabaki akikagua kagua vizuri na kuhakikisha usalama

  Lari alipogeuka kurudi kwenye mto, alimshuhudia Cesy akivua nguo zake na akiingia ndani ya maji kuoga, Lari akafunga macho yake

"Njoo Lari tuoge kwanza!" Binti mfalme alimwita
"Hapana wewe oga tu kwanza!" Lari alimjibu lakini Cesy hakuishia hapo alitoka ndani ya maji akiwa mtupu kama alivyozaliwa na kumshika mkono Lari aliyekuwa akisita sita, akamvuta ndani ya maji akiwa na nguo zake akamshika mikono wakitazamana

"Lari, nipo hapa kwa ajili yako, chukua chochote unachokitaka kutoka kwangu!" Cesy alimwambia wakitazamana machoni

"Hakuna ninachohitaji kutoka kwako zaidi ya kuhakikisha upo salama muda wote bintimfalme!" Lari alimjibu

"Mimi nipo salama nikiwa na wewe!" Cesy aliongea akisogeza mdomo wake taratibu kwenye mdomo wa Lari ambae kama kijana wa kiume mtandao' ulishasoma, akakipokea kidevu cha msichana huyo wakaanza kupeana mate (denda) taratibu wakiwa ndani ya maji ya mto (usawa wa kiuno)

  Mate (denda) yalinoga, Lari akiipitisha mikono yake kiunoni mwa msichana Cesy na kuanza kumpapasa, huku Cesy akivua nguo za kijana huyo na kuzitupia nje ya mto, wote wakabaki kama walivyozaliwa ndani ya maji wakiendelea kupeana mate huku Lari akishuka taratibu mpaka kifuani mwa msichana huyo na kuanza kumnyonya matiti yake taratibu, Cesy akipeleka mkono ndani ya maji na kumshika Jogoo wa Lari akimpapasa papasa

  Walishikana mikono na kutoka ndani ya maji wakasogea mpaka chini ya mti mmoja mkubwa kando ya mto Cesy akauegemea mti akitanua mapaja yake, Lari akapita katikati ya mapaja yake na kumwingiza Jogoo wake taratibu kwenye uchi wa msichana huyo na kuanza kumsugua huku akimbusu busu shingoni na maeneo hatarishi' ya mwili wake, wakiwa wamelowana maji ya mto

"aaaasssss Lariiii!!" Cesy alilalamika kimahaba wakati kijana Lari akizidi kumsugua na akambeba kabisa, kiunoni, miguu ya msichana huyo akaizungushia kiunoni mwa Lari huku wakipeana mate (denda) la nguvu lililojaa hisia kali za kimapenzi


  Lakini wakati wakishea mapenzi yao chini ya mti huo mkubwa, nyoka mkubwa (chatu) alikuwa amejipumzisha amejizungusha kwenye tawi moja la mti huo wao bila kujua, nyoka huyo nae hakuwaona, lakini alipowaona chini akagundua vitoweo vimejileta vyenyewe chini, akajitoa taratibu kwenye tawi alilokuwa amejizonga zonga, akaanza safari ya kuelekea chini ya mti kwenda kujaribu bahati yake.....

  Upande wa pili ndani ya kasri la mfalme (ikulu) mfalme Longe anarejea na msafara wake taratibu wa askari wake, safari hii akiwa mwenyewe tu bila ya mwanadada Susi, shemejie, kutokana na kutoweza kurudi sababu ya kumhofia dada yake, aliyewafumania jana lakini akawaacha na kurejea ndani ya jumba (kasri) la kifalme

  Mfalme alipoingia na kushuka kwenye gari lake (la farasi) alimkuta mkewe, malkia Suze akiwa amekaa bustanini, akamfuata

"Habari yako mke wangu" alimsalimia
"Salama!" mkewe alijibu wakabaki wametazamana, mfalme Longe akainamisha kichwa chake chini kwa aibu huku akijikuna kidogo

"Nisamehe mke wangu nilipitiwa tu!"
"Niko radhi ningekukuta na mwanamke yeyote yule wala nisingekubudhi lakini mdogo wangu damu moja namimi mh hapana sikuelewi!"

"Yamepita mke wangu ni shetani tu alinipitia!"
"Ndiyo Susi ni shetani kweli, lakini bi Redo alinionya sema tu sikumtilia maanani, usijali mume wangu, mimi wala sina tatizo nawewe kabisa ila huyo mwanamke huyo mnafiki wa kunionyesha upendo kwa nje kumbe ananizunguka mgongoni asirudi tena ndani ya jumba hili, labda niwe nimekufa, kama undugu wetu na ufe tu!" malkia Suze aliongea

"Usizungumze maneno makali hivyo Suze yule ni ndugi yako!"
"Wewe shida yako nini kwani, mimi nawewe si tumemalizana, nenda ndani kamsalimie mama amekuja hayo mengine yaache kama yalivyo, nitamalizana mimi mwenyewe na ndugu yangu kama anafikiri umalkia unapatikana kirahisi hivyo atanijua mimi nani, katangaza vita!"

"Oooppps sawa!" mfalme Longe alimjibu mkewe akitembea kinyonge taratibu kuelekea ndani ya kasri

"Susi hahaha, umejitafutia shida ambayo utajutia maisha yako yote!" malkia Suze alijisemesha mwenyewe akitabasamu wakati huohuo waziri mkuu mzee Poso aliingia ndani ya jumba (kasri) la mfalme akiwa na walinzi wake akiwa kana kwamba amechanganyikiwa na kitu, alimkuta malkia Suze bustanini lakini akataka kumpita kana kwamba hajamuona kutokuwa na akili yake kutotulia, lakini malkia Suze akamfuata

"Mbona mbiombio mpaka hatusalimiani tunapitana tu?" malkia Suze alimwuliza
"Samahani malkia kichwa changu hakipo sawa unaendeleaje?"
"Naendelea vizuri tu vipi kuna tatizo lolote?"
"Hakuna tatizo, nahitaji tu kukutana na mume wako samahani!" mzee Poso alimjibu malkia akaendelea na safari yake kuingia kwenye sebule kuu ya mfalme

"Kuna shida gani?" malkia Suze alijiuliza, alipoona mzee huyo waziri mkuu ambae pia ni mjomba wa mumewe mfalme Longe, akiwa mwenye haraka sana, malkia Suze kama kawaida yake huwa hakubali kupitwa na jambo au habari yoyote, nae akaelekea hukohuko ndani kujua kilichotokea

 Mfalme Longe alikuwa chumbani kwake ametulia tuli, akiwaza na kuwazua cha kufanya baada ya kujiharibia mwenyewe,

"Hodi!" mlango uligongwa
"Nani?" mfalme aliuliza
"Mtumishi wako!" jenerali alijibu
"Ingia!" mfalme alimjibu jenerali huyo akaingia chumbani
"Mtukufu mfalme, waziri nkuu anakuhitaji yupo sebuleni ana mazungumzo nawewe!"
"Mwambie aje wakati mwingine sipo sawa sasa!"

"Sawa mtukufu mfalme, lakini amedai ni mazungumzo ya muhimu sana!"

"Nimekwambia mwambie aje wakati mwingine!" mfalme Longe aliongea kwa ukali na hasira
"Sawa samahani mtukufu mfalme!" jenerali alijibu na kurudi nyuma akatoka chumbani mwa mfalme

"Anakuja?" mzee Poso alimwuliza
"Hayupo sawa amesema uje wakati mwingine!" jenerali alimjibu

"Wakati mwingine upi tutakuwa tumeshachelewa nchi itakuwa imeingia kwenye wakati mgumu sana!"
"Wakati upi huo mgumu?" mfalme aliuliza kumbe alishafika
"Ramani imepotea, karatasi ya ramani nimeibiwa!" waziri mkuu alimwambia mfalme Longe ambae alishtushwa na taarifa hiyo

"Imepoteaje poteaje?"
"Nimeibiwa na wezi ndani kwangu!"
"Mjomba sitakusamehe unataka kuiuza nchi yangu!" mfalme alimnyang'anya jenerali upanga na kumnyooshea ncha ya upanga waziri huyo mkuu, mzee Poso ambae ni mjomba wake (kaka wa mama yake, bi. Tusa) akabaki ametoa macho......


Inaendelea!

NCHI YA DHAMBI
SEHEMU YA: 12


    *************

  Leo ilikuwa sikukuu maalumu ya mapenzi katika nchi hii ya Toro ambapo katika siku hii ya leo watu hushinda wakifanya mapenzi tu, iwe mke na mume au wapenzi tu, ruksa kufanya mapenzi popote pale iwe dukani iwe sokoni, watu walikuwa wakibusiana na kupeana denda (mate) na wengine wakishughulikiana kwenye kona za masoko

  Ndani ya gereza kuu la nchi ya Toro lenye wahalifu wakubwa sana, majambazi walioshindikana, jambazi sugu na muuaji aitwae Zenja alikuwa ametulia ndani ya chumba chake maalumu chenye giza totoro, akiwa amehukumiwa kunyongwa siku kadhaa zijazo kutokana na makosa yake makubwa ya mauaji, likiwa ni jitu la miraba minne, katili na asiye na huruma wala kidogo, akipendelea kunyoa upara kichwani akivuta sigara yake taratibu


  Ndipo mlango wa chumba chake alichofungiwa ulipofunguliwa akageuza uso wake wa kutisha na kutazama askari wawili waliokuwa mbele yake

"Mna shida gani?" aliwauliza
"Una mgeni anataka kukuona!" askari mmoja alijibu
"Mgeni gani?" jambazi huyo aitwae Tai aliuliza,

"Mimi hapa!" mwanadada aliingia ndani ya chumba hicho, hakuwa mwingine, alikuwa ni Susi mdogo wa malkia Suze

"Sema shida yako!"
"Nina kazi ndogo tu nataka nikupatie ambayo nitakulipa pesa na kukutoa humu gerezani!" mwanadada Susi alimwambia

"Unitoe humu wewe kama nani?" Tai alicheka kwa dharau maana alikuwa hamfahamu kabisa mwanadada Susi

"Mimi ni shemeji wa mfalme Longe, mdogo wa malkia Suze!" alijitambulisha

"Oooh samahani kumbe ninaongea na mtu mzito hivyo?"

"Bila samahani, upo tayari kwa kazi?"
"Nadhani ni ya kumfyeka mtu siyo?"
"Ndiyo!"
"Nani?"
"Malkia Suze!"
"Malkia Suze si ni dada yako?"
"Hilo lisikusumbue, wewe fanya kazi ninayokutuma!"
"Weka mzigo mezani!" Tai aliongea, msaidizi wa mwanadada Susi akasogea na mfuko ulijaa sarafu (fedha ya wakati huo) akazimwaga mbele ya jambazi huyo sugu

"Kazi itaanza kesho!" mwanadada Susi alimwambia
"Bila shaka!" Tai alicheka baada ya kuona pesa mbele yake

"Mleteeni zawadi nyingine maalumu!" Susi aliagiza wakaingizwa wanadada wawili makahaba ndani ya chumba hicho cha jambazi sugu ambae alipowaona alipagawa akawavuta haraka na kuwavua wanadada hao nguo maana ana miezi mingi hajafanya mapenzi na mwanamke

  Mwanadada Susi alitoka ndani ya chumba hicho huku mayowe ya wale wanadada makahaba yakisikika wakati wakishughulikiwa na yule jambazi aliyekuwa na uchu wa siku nyingi wa kufanya mapenzi na mwanamke

"Una uhakika na unachotaka kukifanya?" msaidizi wa Susi alimwuliza bosi wake huyo

"Nina uhakika, lazima niwe malkia kamili wa nchi hii, sijali itagharimu nini na maisha ya nani yatateketea!" Susi alimjibu msaidizi wake huyo aliyetikisa tu kichwa kukubaliana na bosi wake huyo.......

......

 Upande mwingine...

....

  Makali ya upanga wa mfalme Longe yalikuwa kwenye shingo ya mjomba wake, na waziri wake mkuu, mzee Poso ambae alibaki akitetemeka

"Mume wangu unataka kufanya nini?" malkia Suze alipoona alisogea kujaribu kuituliza hasira ya mumewe huyo

"Ameshaiuza nchi huyu mzee ile ramani ni kitu cha muhimu sana sasa kipo mikononi mwa maadui, siku siyo nyingi tunavamiwa na kutawaliwa, ile ramani ilibidi tuitumie sisi tuwatawale wengine wote, lakini sasa tunakwenda kutawaliwa, muda si mrefu na hao wa nchi waliyoiiba, kwenye ile ramani kuna hazina kubwa ambayo waliyoichukua wakiipata basi tumekwisha, wataitawala kila nchi, ile ramani ipo tangu enzi na enzi, unayajua hayo yote?" mfalme alimwuliza mkewe, malkia Suze kwa hasira akiwa bado amemnyooshea upanga mjomba wake, waziri mkuu mzee Poso ambae alikuwa amepiga magoti akitetemeka

"Kuna nini kinaendelea kulikoni mbona umemnyooshea upanga mjomba wako??" bi. Tusa alitokea akishangaa kukuta kaka yake, Poso amenyooshewa upanga na kijana wake, Longe

Mfalme Longe akabaki ametazamana na mama yake, bi. Tusa, macho kwa macho, uso kwa uso, kukapita ukimya wa sekunde kadhaa.....

"

   Upande mwingine

"Aaaaaasssss Lari uuwiiiii!" msichana Cesy alikuwa amemkalia Jogoo' wa kijana Lari, askari mlinzi wa mama yake, malkia Suze akimpa penzi huku akiguna kimahaba, wawili hao wakiwa chini ya mti mkubwa pembezoni mwa mto

 Lari alibaki amekishikilia kiuno cha mwanadada huyo safari hii akiwa amechuchumaa na kumpakata msichana huyo huku akimnyonya matiti yake kifuani akiendelea kumsugua kwa Jogoo' wake aliyezama wote kwenye uchi wa msichana huyo


  Bila ya wao kujua kinachoendelea nyuma yao, nyoka mkubwa (chatu) aliteremka kwenye mti taratibu wakati vijana hao wakiwa wamezama penzini

 Msichana Cesy alishusha pumzi ndefu alipofunga bao akamng'ang'ania Lari akimpa mate (denda) Lari nae alimaliza kwa kushusha mzigo' ndani ya uchi wa msichana huyo, wote wakabaki wakihema kwa kasi

"Asante Cesy!" Lari alimwambia
"Asante nawewe Lari, nakupenda sana sana!" Cesy alijibu wakainuka na kusimama wakakumbatiana taratibu na kupeana mate (denda) tena

 Lari alitembea hatua chache kufuata nguo zao pembeni mwa mto Cesy akabaki ameuegemea mti akitabasamu huku mkono wake akijishika shika kwenye uchi' wake

  Lakini mara ghafla akajikuta nyoka mkubwa (chatu) akijiviringisha shingoni mwake Cesy akashtuka na kupiga kelele zilizomshtua kijana Lari aliyegeuka akiwa na nguo zao mkononi na kurudi akashuhudia msichana huyo akiwa amezingwa zingwa na chatu huyo kuanzia kiunoni mpaka shingoni, chatu akiachama kichwa chake kutaka kummeza......


Inaendelea!NCHI YA DHAMBI
SEHEMU YA ~ 13


    ************
  Macho ya mfalme Longe yalikuwa yakitazamana na mama yake mzazi, bi Tusa, huku upanga wake ukiwa kwenye shingo ya kaka huyo wa mama yake (mjomba) waziri mkuu mzee Poso

 Mfalme Longe aliurudisha upanga kwa jenerali mjomba wake huyo akashusha pumzi ndefu baada ya kunusurika kukatwa shingo na mpwawe huyo ambae alijawa na hasira

"Unadiriki kumtishia maisha mjomba wako?" mama yake alimwuliza
"Samahani mama, alilolifanya hata kama ningemkata kichwa chake nisingesikitika pamoja na kuwa ni mjomba wangu!" mfalme alimjibu mama yake huyo, wakabaki wametazamana tu

"Sawa basi ni vyema kila mmoja akaituliza hasira yake ili amani ya nyumba hii irudi tena!" malkia Suze aliongea na wakati huo huo wakamwona askari Jeda akiingia sebuleni akiwa na jeraha kichwani

"Mtukufu mfalme!" askari huyo aliongea akipiga magoti mbele ya mfalme Longe na malkia Suze

"Kuna tatizo gani na umetokea wapi na vipi hayo majeraha?" malkia Suze alimwuliza

"Mtukufu malkia, nimetoka kujaribu kumuokoa binti yenu Cesy bila mafanikio yupo katika hatari, nimeshindwa!"

"Cesy, kwenye hatari gani kwani hayupo humu ndani?"

"Hayupo tangu jana mtukufu malkia!" askari Jeda alijibu
"Imekuwaje kuwaje?" mfalme Longe aliuliza, wote walikuwa hawana habari za binti yao, huenda kutokana na mitafaruku iliyokuwa ikiendelea ndani ya jumba (kasri) hilo, wakajikuta hawana habari ya binti yao wakijua tu yupo ndani ya kasri

"Ni jana alitoroshwa ndani ya kasri!" askari Jeda aliongea
"Na nani?" malkia Suze alimwuliza
"Na askari mlinzi wako, Lari!"

"Lari????!!!" malkia Suze alishikwa na butwaa
"Unapafahamu alipo?" mfalme alimwuliza
"Ndiyo mtukufu mfalme wapo maeneo ya mtoni, porini!"

"Mnasubiri nini, tuma askari kikosi kizima wakamkamate huyo askari na wamlete binti yangu hapa akiwa hai!" mfalme alitoa amri

"Ndiyo mtukufu mfalme nitafanya hivyo sasa!" jenerali mlinzi mkuu wa mfalme aliitikia akiinamisha kichwa chake na kugeuka haraka haraka kwenda kufanya alichoamriwa

"Nitafuatana nao nikajue imekuwaje kuwaje!" malkia Suze aliongea nae akiondoka haraka haraka kufuatana na kikosi hicho cha askari kwenda kumfuata bintiye Cesy, mfalme akibaki anajikuna kichwa akiwa anatembea tembea mwenyewe kila mtu ndani ya kasri akiwa kimya akitafakari yanayoendelea ndani ya jumba (kasri) hilo kubwa la kifalme ambalo lilikuwa na kila kitu ndani vyakula vya kila aina, mapambo na samani za kila aina za madini na za kuvutia, lakini kilichokosekana ni amani tu......

.....

  Upande mwingine kijana Lari alikuwa akimtazama msichana bintimfalme Cesy aliyekuwa amezongwa zongwa na chatu mkubwa aliyeachama kinywa kutaka kummeza

"Lari nakupenda hata nikifa uniagie kwa mama!" Cesy aliongea maana alijua kwa vyovyote hawezi kutoka kwa chatu huyo mkubwa

"Haufi Cesy niachie mimi!" Lari alimuhakikishia msichana huyo na akaondoa woga na kumsogelea palepale

"Hapana Lari usije!!" Cesy alimpigia kelele, chatu alipoona anataka kuingiliwa kwenye kitoweo chake akageuza kichwa chake kumtazama mtu anayetaka kumuharibia mawindo yake hayo aliyoyapata kiulaini kabisa

  Lari hakuogopa akaokota mti na kusogea karibu, kisha akamsukuma msichana Cesy kwa nguvu, msichana huyo akaanguka mzima na chatu akiwa amemzongazonga, ndipo chatu akajitoa kwenye mwili wa msichana Cesy kwa hasira na kuanza kumfuata kijana Lari aliyekuwa na kipande cha mti, Lari akaanza kurudi nyuma nyuma wakati chatu huyo akiinua kichwa chake kisha akaruka mzima mzima na kuudaka mkono wa kijana Lari akaung'ang'ania, Lari akiwa ameshika kipande cha mti mkono mwingine akamtandika Chatu huyo aliyegoma kuuachia mkono wake mpaka akamtoboa kwa kipande hicho cha mti kwenye kichwa chake chatu huyo akauachia mkono wa Lari na kuanguka, msichana Cesy akaja kusaidia akiwa na jiwe gumu mkononi (jabali) akamtandika chatu kichwani na kumponda ponda mpaka chatu huyo akafa papohapo

"Upo salama Lari?" msichana Cesy alimkimbilia kijana Lari na kumkumbatia
"Nipo salama!" Lari alijibu huku akiwa amejishika mkono wake uliokuwa umetobolewa meno makali ya chatu yule huku damu zikimvuja akaona kizunguzungu cha ghafla na kuanguka chini mzima mzima

"Lari Lariii!!!" msichana huyo alimwita Lari akimwona sura yake kwa mbali kutokana na macho yake kukosa nuru kutokana na sumu ya nyoka iliyoingia mwilini mwake alipoumwa meno......


    Kijana Lari alikuja kuzinduka akijikuta yupo kwenye nyumba ya yule bibi kizee, na msichana Cesy akiwa pembeni yake

"Bibi ameamka!" Cesy alishangilia
"Nimekuambia mimi dawa niliyomnywesha lazima sumu iondoke apone!" bibi kizee alimwambia msichana Cesy ambae alimsogelea Lari

"Unajisikiaje sasa?" Cesy alimwuliza
"Vizuri tu kimetokea nini?"
"Uliumwa na yule chatu ila bahati nzuri bibi alipita akiwa ameghairi safari yake akatukuta, akakuwahi na kukunywesha dawa ulipokuwa umepoteza fahamu!" Cesy alimwelezea Lari akatikisa kichwa akijitazama mkono wake ukiwa umepakwa pakwa unga unga wa kijani (dawa)


"Wruuuuuuuuu!!" mara nje wakasikia milio na vishindo vya farasi

"Farasi hao wanatokea wapi huku porini?" bibi alijiuliza na kutoka nje akakuta askari wameizingira nyumba yake ya kibanda na malkia Suze akishuka juu ya farasi wake, bibi kizee akainama (kutoa heshima)

"Unaishi na nani humu porini?" malkia Suze alimwuliza
"Naishi peke yangu mtukufu malkia, kulikoni ugeni huu wa heshima kuja kwangu leo mimi nisiyefaa kitu kuna tatizo gani?"

"Namtafuta binti yangu Cesy amekuja huku porini kwenye mto na kijana askari wa kiume aliyemteka!"

"Sijawaona mtukufu malkia!" bibi kizee alijibu akiwa hajui kuwa wageni alionao ndio malkia anaowatafuta, muda huo msichana Cesy na kijana Lari walikuwa wametulia ndani wakisikiliza kwa makini kinachoendelea

"Una uhakika na unachokisema?"
"Ndiyo mtukufu malkia kuna vijana wawili tu wageni wangu walionisaidia lakini siyo bintimfalme wala mwana wa mfalme!"

"Hebu watoe nje niwaone!" malkia alimwambia bibi huyo

"Ni mimi hapa mama!" Cesy aliamua kujitokeza mwenyewe malkia akamshangaa na kumfuata na kumkumbatia

"Binti yangu!"
"Kumbe wewe ni binti mfalme?" bibi kizee alishikwa na bumbuwazi, wakati huo kijana Lari akaamua kujitokeza nae uso kwa uso akatazamana na malkia Suze

"Mkamateni huyo mtekaji na msaliti!" malkia aliwaamuru askari

"Hapana mama!" Cesy alimzuia mama yake, lakini hakumsikiliza, askari wakampiga kwanza kijana Lari na kumfunga kamba ya chuma (pingu) huku askari Jeda akitabasamu

"Hatimae sasa umeingia kwenye kumi na nane (18) zangu" askari Jeda adui mkubwa wa kijana Lari aliongea kimoyomoyo......


InaendeleaNCHI YA DHAMBI
SEHEMU YA ~ 15 (MWISHO)


  ************

  Lari alimfungua farasi mmoja wapo aliyekuwa kwenye gari la malkia lililoanguka na kuwapakiza malkia Suze na bintiye Cesy na yeye mwenyewe akapanda, jambazi Tai alipoona wanataka kutoroka akairusha nyundo yake kubwa iliyoruka

"Inameni!" Lari aliwaamrisha malkia Suze na bintiye Cesy wakainamisha vichwa vyao nyundo hiyo kubwa na nzito ikawapitia vichwani ikkwakosa kosa wote watatu na farasi akaanza kukimbia akiwa amewabeba watu watatu mgongoni, malkia Suze, bintiye Cesy na kijana Lari

"Wafuatenii!" jambazi Tai aliwaamrisha watu wake nao wakapanda juu ya farasi baada ya kuwamaliza askari wote wa msafara wa malkia Suze na kujaribu kuwakimbiza......

  Lango kuu la jumba (kasri) la mfalme linafunguliwa, na anaingia farasi akiwa amebeba watu watatu mgongoni, mfalme Longe aliyekuwa bustanini amepumzika anasimama na kushangaa, mkewe Suze na bintiye Cesy pamoja na kijana Lari wanashuka juu ya farasi

"Mkamateni huyo askari muasi!" mfalme anawaamuru askari wanaosogea haraka haraka na kumshika Lari

"Hapana mwacheni siyo yeye aliyehusika" malkia Suze anawazuia wasimkamate

"Mpo salama mbona mmerudi wenyewe bila ulinzi wowote?"

"Tumevamiwa njiani askari wameuwawa!"

"Mmevamiwa na nani??" mfalme aliuliza akiamrisha vikosi viwili vya askari vilivyotoka haraka haraka nje ya kasri kwenda kuwashughulikia wavamizi hao huku malkia Suze akimsimulia tukio lote jinsi lilivyokuwa wakati wakizungumza hayo askari wawili walikuja mbio mbio wanaokaa juu kwenye kuta za nchi hiyo wakiangalia usalama wa mipaka

"Mtukufu mfalme tumevamiwa!" walipiga kelele wakija na kuinamisha vichwa vyao mbele ya mfalme Longe

"Tumevamiwa na nani?" mfalme aliwauliza
"Jeshi kubwa la nchi ya Mashariki tumeliona likija karibu na mipaka yetu kwa jinsi walivyo jeshi kubwa sidhani kama tutabaki salama!"

"Piga baragumu itisha vita!" mfalme aliamuru akitembea haraka haraka kuingia ndani ya sebule yake ndani

 "Cesy jichunge jifiche!" Lari alimwambia binti mfalme akimbusu shavuni

"Wewe unaenda wapi sasa?" Cesy alimwuliza akiogopa baada ya kusikia habari ya vita

"Naingia vitani, umesahau mimi ni askari!" Lari alimjibu Cesy akimbusu mdomoni na kumuacha akakimbia kuungana na askari wengine katika maandalizi ya kukabiliana na jeshi kubwa la nchi ya Mashariki linalokuja kuwavamia

"Lariiii!" Cesy alinyoosha mkono akiita

Mama yake malkia Suze alikuwa pembeni akitazama akishuhudia mapenzi hayo baina ya bintiye huyo na kijana Lari, akiumia maana na yeye alimpenda kijana Lari na ameshaonja penzi la kijana huyo, ndani ya kasri taharuki itawala kila mtu akijaribu kutafuta namna ya kuokoa maisha yake kutokana na vita inayokaribia huku jeshi la nchi ya Mashariki likiingia kwenye mipaka ya nchi ya Toro kwa kasi ya kimbunga....


  Upande mwingine mwanadada Susi alikuwa nyumbani mwake akisubiri ripoti ya kazi yake ya kumuua dada yake, malkia Suze ambayo alimpa jambazi sugu, Tai pamoja na kundi lake

  Mlango wake uligongwa akainuka na kuufungua, akakutana uso kwa uso na jambazi Tai

"Vipi kazi yangu imefanikiwa?" alimwuliza jambazi huyo
"Imefanikiwa kiasi!"
"Kivipi?"
"Tumewaua askari wote wa malkia!"
"Na malkia je?"
"Ametoroka!"
"Ametoroka kivipi na mmewezaje kuwaua askari mkamwacha atoroke!"

"Ni makosa tu katika kazi!" jambazi Tai alimjibu

"Makosa tu katika kazi, unanijibu kirahisi rahisi tu wakati mmekula pesa nyingi na kazi hamjaitimiza?"

"Usijali itapatikana nafasi nyingine tu kazi yako itafanyika!"

"Nafasi nyingine, wapumbavu ninyi!" Susi aliongea kwa ukali jambazi huyo akamkamata mkono na kumvuta kifuani mwake kisha akamkaba shingoni, Susi akabaki akifurukuta

"Unajiona wewe nani mpaka uthubutu kunitukana mimi na watu wangu, naweza kukunyonga hapahapa ukawa ndio mwisho wako malaya wewe!" jambazi Tai alimnong'oneza mwanadada Susi Sikioni

"Baasii niachie unaniumiza nakosa pumziiii!!" Susi alilalamika akirusha rusha miguu kwa kukosa hewa wakati huohuo msaidizi wake aliingia mbiombio bila hodi akikimbia akiwa ametokea sokoni na kapu lake mkononi akakuta bosi wake amekabwa

"Tafadhali naomba muachilie bosi wangu!" alimsihi jambazi Tai

"Siku nyingine asirudie kutukana watu ovyo!" Tai alijibu akamwachia mwanadada Susi ambae aliinama na kukohoa mfululizo kutokana na kukosa pumzi

"Jamani kila mtu ajiokoe maisha yake nchi imevamiwa!" mtumishi huyo aliwaambia

"Imevamiwa kivipi?" Tai alimwuliza
"Jeshi la nchi ya Mashariki limeshaingia ndani ya nchi yetu tayari kwa vita nimeona sokoni nilipokuwa nanunua vitu!" mtumishi huyo aliongea Tai na mwanadada Susi wote wakatoka nje na kukuta taharuki kila mtu akikimbia kimbia, hata watu wake walishakimbia muda mrefu hakuna aliyebaki

"Ngoja nielekee huku!" jambazi Tai aliongea akikimbia

"Tumekwishaa!" mwanadada Susi alibaki amejishika mikono kichwani nae akikimbia asipopajua na msaidizi wake akakimbia upande mwingine, kila mtu ndani ya nchi ya Toro akabaki akikimbia kujaribu kuyaokoa maisha yake, wakati huo jeshi kubwa na lenye nguvu la nchi ya Mashariki likiwa limeshaingia ndani ya nchi hiyo ya Toro na kuizunguka......


MWISHO WA SEASON 01

Kaa tayari,
SEASON 02 itakujia hivi karibuni

usiige matendo ya kwenye simulizi hii
ni burudani tu na siyo kisa halisi
ukimwi unaua

Asante kwa kuifuatilia na kuinunua

                 Like share comment  
   
Reactions

Chapisha Maoni

0 Maoni

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();