Ticker

6/recent/ticker-posts

SABABU ZA TATIZO LA KUTOPATA MIMBA NA TIBA ZAKE



SABABU ZA TATIZO LA KUTOPATA MIMBA NA TIBA ZAKE


Tatizo la kutopata mimba linawasumbua wengi na huwapata familia kadhaa katika jamii, huweza kumpata mtu mmoja kati ya wanandoa 12 na ni tatizo linalowapata watu zaidi ya milioni 24 duniani kote.

Ugumba ni hali ya kutoweza kupata ujauzito katika kipindi cha mwaka mmoja au zaidi kwa wenzi ambao wamekuwa wakifanya mapenzi bila kutumia njia zozote za uzazi wa mpango. Mtiririko wa upataji ujauzito ni kama ifuatavyo;

Baada ya mwezi mmoja wa ndoa uwezo wa kushika ujauzito ni asilimia 20, baada ya miezi mitatu ya ndoa ni asilimia 50, baada ya miezi sita ya ndoa ni asilimia 75 na baada ya miezi 12 ni asilimia 90 mwanamke huweza kupata ujauzito.

Hali hii inaweza kutokea kutokana na tatizo kwa mwanaume au mwanamke, ingawa baadhi ya watu wamekuwa wakidhani wanawake peke yao ndio ambao hupata tatizo hilo.

Tatizo hili limegawanywa katika vipengele viwili kimoja ni kile ambacho mwanamke hushindwa kupata mimba baada ya mwaka mmoja wa kufanya tendo la ndoa na mume wake bila kutumia kinga kwa mwanamke mwenye umri chini ya miaka 35 (primary infertility).

Kipengele cha pili ni kile kijulikanacho kama 'secondary infertility' ambapo mwanamke hushindwa kubeba mimba wakati siku za nyuma alishawahi kupata ujauzito.

Tatizo la ugumba huweza kupatiwa matibabu na kuisha.

KUNA TAFAUTI GANI KATI YA UGUMBA NA UTASA?

Tofauti na ugumba, utasa ni hali ya mwanamke kutoweza kushika ujauzito kabisa au mwanaume kutoweza kusababisha ujauzito kwa mwanamke kabisa.

Mtu tasa hana uwezo wa kupata mimba au kumpa mwenzi wake mimba kabisa, wakati mgumba ana uwezo wa kuja kupata mimba iwapo tatizo litaondolewa.

NINI HUSABABISHA UGUMBA?

Kuna sababu mbalimbali ambazo hupelekea ugumba kutokea kwa mwanaume au mwanamke.

WANAUME
Ugumba kwa wanaume hutokana na tatizo katika mbegu za kiume, manii kuwa kidogo, manii kushindwa kutembea, manii kuwa na umbo lisislo la kawaida au kuziba kwa mijira ya mbegu za kiume.

Tatizo kwenye mbegu za kiume linaweza kutokana na;

- Uvutaji wa sigara
- Dawa za kulevya kama matumizi ya bangi kwa wingi,
- Mionzi (radiations)
- Unywaji wa pombe
- Kemikali kama DDT, risasi (lead)
- Kufanya kazi mazingira yenye joto kali kama viwanda vya chuma.
- Kuziba kwa mirija ya mbegu za kiume kutokana na magonjwa ya zinaa


WANAWAKE
Tatizo la ugumba husababishwa na sababu kuu mbili:

- Kuziba kwa mijrija ya kupitisha mayai
- Ovari kushindwa kutoa mayai ya uzazi au kutoa mayai isiokuwa na nguvu (lazy egg).

Mirija ya kupitisha mayai inaweza kuziba kutokana na;

- Ugonjwa wa Pelvic Inflammatory Disease (PID) ambao unatokana na magonjwa ya zinaa yasiyotibiwa kama kisonono na klamidia.
- Mirija ya mayai kujaa maji
- Utoaji mimba usio salama (unsafe abortions)
- Upasuaji maeneo ya kiunoni
- Ugonjwa wa endometriosis

Ovari kushindwa kutoa mayai ya uzazi inaweza kutokana na;

- Umri mkubwa wa mwanamke, hasa miaka 35 – 40 na kuendelea.
- Uvutaji wa sigara
- Saratani ya Ovari
- Mionzi (radiations)
- Ugonjwa wa Polycystic ovarian disease (Ovarian Cyst)

Sababu nyingine za ugumba kwa mwanamke zinaweza kuwa;

- Makovu katika mji wa uzazi kutokana na kutoa mimba.
- Mabonge ya kizazi (uterine fibroids)
- Kuziba kwa shingo ya uzazi
- Kulegea shingo ya uzazi
- Kisukari
- Matatizo ya tezi ya shingo (hyperthyroidism)
- Kufanya mazoezi ya kupitiliza (excessive exercising)

VIPIMO VYA KUJUA UGUMBA

Vipimo mbalimbali vinapatikana ili kuwezesha kugundua chanzo cha ugumba. Licha ya uwezo wa vipimo hivi, zaidi ya asilimia 10 ya watu wenye tatizo hili chanzo kinaweza kisijulikane kabisa. Ni vizuri kwa wenzi wote wawili wenye tatizo hili kuonana na daktari kwa ajili ya ushauri na vipimo.

KWA WANAUME HUFANYIKA;

Kipimo cha manii (seminalysis) kuona kama manii zipo za kawaida na kwa kiwango kinachoatakiwa. Manii huchukuliwa kwa kondomu maalum wakati wa kufanya mapenzi au kwa kupiga punyeto na kisha kuchunguzwa kwa darubini.

Homoni za kiume kwenye damu; kipimo hiki hupima homoni za testosterone na Follicle Stimulating Hormone(FSH) ambazo huusika katika utengenezaji wa mbegu za kiume.

KWA WANAWAKE KUNA VIPIMO VINGI HUWEZA KUFANYIKA VIKIWEMO;

- Hysterosalpingography – hutazama mirija ya uzazi (Fallopian tubes) kama imeziba au la. Pia huonesha kama tumbo la uzazi lina vivimbe.

- Ultrasound – kipimo hiki huonesha kama kuna vivimbe kwenye tumbo la uzazi, pia kwenye ovari kama kuna magonjwa yanayoweza kusababisha ugumba kama Polycystic Ovarian Syndrome.

- Homoni za kike katika damu – kipimo hiki hupima homoni za 'Oestrogen' na 'Follicle stimulating hormone' ambazo huusika kwenye kuandaa yai la uzazi kutoka kwenye ovari na upandikizaji kwenye mji wa uzazi.

- Endometrial biopsy – tishu za mji wa uzazi huchukuliwa kuchunguza kama yai la uzazi limetoka. Pia huweza kuonesha kama kuna saratani ya mji wa uzazi au vinyama kwenye mji wa uzazi.

MATIBABU YA UGUMBA

Matibabu ya ugumba huhusishwa wenzi wote wawili, mwanaume na mwanamke. Yanahitaji uvumilivu na uelewa kwani wakati mwingine yanaweza yasiwe na mafanikio haraka au kabisa kama tunavyotarajia. Kuna njia mbalimbali za kutibu ugumba, hizi zote zikijumuisha kuondoa tatizo linalosababisha mimba ishindwe kutunga au kutumia njia za kusaidia mimba itunge.

Njia za matibabu ya ugumba hujumuisha:

UPASUAJI 
Mirija iliyoziba, vivimbe kwenye mji wa uzazi au kuta za uzazi kushikamana huweza kutibiwa kwa njia za upasuaji. Matibabu haya husaidia kuongeza uwezekano wa wenzi kupata mtoto.

DAWA
Mirija iliyoziba, vivimbe kwenye mji wa uzazi au kuta za uzazi kushikamana huweza pia kutibiwa kwa Dawa mara nyingine. Matatizo ya ugumba yanayotokana na ovari kushindwa kutoa mayai ya uzazi huweza kutibiwa kwa dawa pia. Dawa hizi hutumika kuziwezesha ovari kutoa mayai ya uzazi ili yawe tayari kurutubishwa. Mara nyingi huweza kusababisha kutoa mayai mengi katika mzunguko mmoja na kusababisha ujauzito wa watoto wengi (mapacha au zaidi) pale yanaporutubishwa.


TEKNILOGIA SAIDIZI ZA UZAZI (Assistive Reproductive Technologies).

Hizi ni njia za kitaalamu ambazo zinatumika kusaidia wenzi kupata ujauzito kutokana na tatizo kwa mwanaume au mwanamke. Njia hizi ni kama 'Artificial Insermination' na 'In Vitro Fertilization'.

- Artificial Insermination; Njia hii hutumika pale ambapo mbegu za kiume zipo kwa kiasi kidogo. Mbegu za kiume hukusanywa na kuingizwa kwenye mji wa uzazi kwa njia za kitaalamu.

- In Vitro Fertilization; Njia hii hutumika hasa pale mirija ya mwanamke imeziba kabisa. Mayai na mbegu za kiume hukusanywa kitaaalamu na kisha yai kuchavushwa. Baada ya hapo yai lililochavushwa hupandikizwa kwenye mji wa uzazi.

Ugumba huathiri wanaume kwa wanawake wa kiwango kinachofanana, hivyo ni muhimu kwa wenzi wote wawili kushiriki katika matibabu.

Ugumba huathiri wenzi wengi kisaikolojia kwa kuleta hasira, majuto, msongo wa mawazo na hata kusababisha mvurugano katika mahusiano yao. Katika nchi zetu za kiafrika, wanawake wamekuwa wahanga wakubwa wa tatizo hili. Ni vizuri wenzi washirikiane katika hili, kwa kupeana moyo na kufuatilia matibabu kwa pamoja. Matibabu yanaposhindwa kabisa kuleta mafanikio, wenzi wanaweza kuasili mtoto/watoto kama watakuwa na utayari.

Mwisho wa makala asante kwa kusoma mpaka mwisho wa makala yetu karibu kwa maswali maoni na ushauri ikiwa una tangazo unahitaji tukutangazie Humu Bonyeza hapa Wasiliana nasi kwa Email 

*BADILI MAISHA*

*Ukitaka kufahamu njia ya kutengeneza Dora 100  mtandaoni kwa mtaji wa Sh:35,000 njoo inbox nikupe huo mchongo*Whatsapp 

kama bado huna App ya MAHABA tafadhali Download kuendelea kupata masomo yetu👇
Reactions

Chapisha Maoni

0 Maoni

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();