Ticker

6/recent/ticker-posts

SIO POA; KAMA UNA MPANGO NAYE MUONYESHE ACHA KUMUWEKA NJIA PANDA!

SIO POA; KAMA UNA MPANGO NAYE MUONYESHE ACHA KUMUWEKA NJIA PANDA!

Kama uko kwenye mahusiano na mdada wa watu, ashafikisha miaka 28 kuendelea, kama unampenda kweli na una mpango wa kumuoa, hembue mueleze na mueleze na mipango yako. Mfanye awe na uhakika kabisa kuwa yeye ni wako, aisee wadada wakishavukaumri wa miaka 27 wanapaniki sana, wanachachawa na wanachotaka kwa wakati huo ni ndoa.

Sasa kama upo naye na hueleweki eleweki basi jua kuwa akitongozwa ni rahisi kukuacha hata kama anakupenda. Mtu umekaa naye miaka mitano bado unamchunguza nini, hata kama humuoi kwa wakati huo ila una mpango wa kumuoa hembu muonyeshe kuwa unampenda na yeye ndiyo utakayeingia naye kwenye ndoa.

Alivyo ndiyo hivyo hivyo, hakuna kipya utakachogundua kwake. Kuna wadada wamepaniki wanaachana na watu ambao ukiongea nao unajua kuwa hao wanaume wanawapenda sema tu hawajafunguka. Ndugu yangu kumchunguza gani huko.

Kama vipi basi mpige ultrasound uone na maini, figo mpaka utumbo na mapafu kwakua tabia hutagundua kipya. Acha kumtesa dada wa watu na kumfanya afikiirie kumkubali mwanaume ambaye hampendi kwakua tu hueleweki kama uko naye au bado upoupo! Kwao wanampigia kelele, majirani, marafiki na wewe hueleweki halafu akikubali mtu mwingine unamuona malaya! Sio poa!

Mwisho wa makala  asante kwa kusoma mpaka mwisho wa story yetu karibu kwa maswali maoni na ushauri ikiwa una tangazo unahitaji tukutangazie Humu pia

*BADILI MAISHA*

*Ukitaka kufahamu njia ya kutengeneza Dora 100  mtandaoni kwa mtaji wa Sh:35,000 njoo inbox nikupe huo mchongo*Whatsapp 

kama bado huna App ya MAHABA tafadhali Download kuendelea kupata masomo yetu👇

 

Reactions

Chapisha Maoni

0 Maoni

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();