Ticker

6/recent/ticker-posts

WANAUME WANATAFUTA UTII NA WANAWAKE WANALILIA UPENDO WA DHATI JE NI UPANDE UPI UKUBARI KUWA SEHEMU YA HITAJI SAHIHI LA MWENZA WAKE

 


WANAUME WANATAFUTA UTII NA WANAWAKE WANALILIA UPENDO WA DHATI JE NI UPANDE UPI UKUBARI KUWA SEHEMU YA HITAJI SAHIHI LA MWENZA WAKE

Safari ya kila mtu kutafuta kile MUNGU aliagiza Katika ndoa kwamba;-

👉🏼 MWANAUME AMPENDE MKE WAKE💯

👉🏼 MWANAMKE AMTII MUME WAKE💯

Hicho ndicho kinawagharimu wengi hata kujikuta wanakosa maana halisi ya ndoa, Mwanamke katika kutafuta Mwanaume mwenye UPENDO ambaye atambembeleza na kumpa kila atakacho imewaingiza wanawake wengi katika matatizo ikiwemo kuwa na orodha kubwa ya wanaume, kuzalishwa ama kuolewa na watu ambao hawakuwa katika ndoto zao🤦🏻‍♂️

Wanaume nao katika kuhangaikia UTII wa Mwanamke wamejikuta wanaharibu watoto wa watu kwa kuwapa mimba na wengine kuwaoa kisa tu ya kujua mapenzi na mwisho kabisa wanawapa nafasi ndogo katika maisha yao😭

Kwenye kumtafuta mwenza ambaye anatakiwa kusimama katika eneo lake husika hakuna VIGEZO📍

Bin adam wanaonekana zaidi nje ila uhalisia wao umejificha ndani ni wakati gani utaujua hilo ni fumbo, Ndo maana Wengi wanaanguka ama kuumia kwa kujaribisha ndoa badala ya kupambana kutafuta uhalisia wa mtu mkiwa kwenye mahusiano, Mahusiano sio lazima kwenda kitandani kufanya mapenzi, Mahusiano ni ujenzi wa UPENDO kuelekea NDOA💯

Mambo ya kutaka kujua kama anafaa kuwa Mume ama mke kwa kushiriki nae ki mwili ni kudhoofisha Safari yenu katika NDOA🗣️

Mara nyingi wanandoa waliotokea kwenye mahusiano ya kujuana ki mwili kabla ya ndoa yao husababisha mazoea ambayo huathiri uimara wa ndoa, Kuna shauku ya MAPENZI na shauku ya NDOA hayo yanaua maana halisi ya UPENDO 🕺🏻

Siku zote ngono ikitangulia mbele huuacha UPENDO nyuma na kwa vyovyote vile ni ngumu kwa mtu kuijua tena maana ya UPENDO💯

Kuijenga ndoa imara na yenye mfano kwa wengine ni rehema ya MUNGU kwa mmoja kukubari yeye awe sababu ya hitaji la mwenza wake, Hapatakuwa na muujiza wa kupata FURAHA NA AMANI kama kila mmoja atalazimisha apate atakacho, Kwenye ndoa bora hakuna uwiano lazima upande mmoja utatakiwa kuwa dhaifu, Na alindaye ndoa kuwa IMARA ni Mwanamke, Mwanamke akifanikiwa kumtii Mume basi hata mume awe mjinga kiasi gani ndoa itakuwa mfano wa wengine, Mwanaume mpe UPENDO WA DHATI 💘 Mkeo kwani hakuna gharama katika hilo, na ndani yake UTAFURAHIA kila kitu😋

Mwisho wa makala  asante kwa kusoma mpaka mwisho wa story yetu karibu kwa maswali maoni na ushauri ikiwa una tangazo unahitaji tukutangazie Humu pia

*INGIZA SH:250,000 KWA MTAJI WA  SH:10,000*

*Fahamu jinsi ya kuingiza mpaka Tsh:250,000 Kwa mtaji wa Tsh:10,000 kupitia smartphone  njoo inbox nikupe huo mchongo*Whatsapp 

kama bado huna App ya MAHABA tafadhali Download kuendelea kupata masomo yetu👇
Reactions

Chapisha Maoni

0 Maoni

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();